• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara (MMM) |
    • Barua Pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Mbinga Town Council
Mbinga Town Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikao na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Mbinga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi ya Maadili
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi
      • Uchaguzi
      • Nyuki
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Afya
      • Mipango Miji na Maliasili
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo na Umwagiliaji
    • Ufugaji
    • Viwanda
    • Mawasilianao na Usafirishaji
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za maji
    • Huduma za watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
    • Ofisi ya Mbunge
  • Miradi
    • Inayotekelezwa
    • Iliyotekelezwa
    • Inayotarajia kutekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Sheria ndogo
    • Fomu mbalimbali
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Video
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
  • Shule
    • Shule za Msingi
    • Shule za Sekondari
      • Agustivo High School
      • Dr. Shein Secondary School
      • Makita Secondary School
      • Luhuwiko Secondary School
      • Mbinga Secondary School
      • Mbambi Secondary School
      • Mikiga Secondary School
      • Mbangamao Secondary School
      • Kikolo Secondary School
      • Kagugu Secondary School
      • Ndela Secondary School
      • Ngwilizi Secondary School
      • LAMATA Scondary School
      • Kindimba Secondary School
      • Lusetu Secondary School
      • Depaul Mbangamao Secondary School
      • Mkwaya Secondary School

HALMASHAURI YA MJI WA MBINGA YADHAMIRIA KUBORESHA LISHE SHULENI

Tarehe ya kuwekwa: August 18th, 2023

Mbinga. Katika juhudi ya kutekeleza agizo la utoaji wa vyakula vyenye virutubisho shuleni, Halmashauri ya Mji wa Mbinga (MTC) jana Agosti 17 ilifanya kikao na wamiliki wa mashine za kuzalisha unga pamoja na SANKU---mtoa huduma katika programu ya kuchanganya virutubishi kwenye unga wa mahindi.

Kikao kilicho wakutanisha SANKU pamoja na wamiliki wa mashine za nafaka kutoka kata nane za Mbinga Mji kililenga kihamasisha wana Mbinga Mji kuwa na mashine nyingi za kuchanganya virutibishi kwenye unga wa mahindi.

Akizungumza wakati wa kikao msimamizi wa kanda wa SANKU Christian Lutaja alisema mashine na virutubishi hotolewa bure na kwamba wahitaji wanachotakiwa kufanya ni kununua mifuko tuu.

"Oda ya kwanza inatakiwa isipungue mifuko 2,000," alisema bwana Lutaja.

Alisema mfuko wa kilo 5 huuzwa kwa Sh475, wakati kilo 50 ni Sh900.

Katika mkoa wa Ruvuma tayari mashine 30 za kuchanganya virutubishi kwenye unga wa mahindi zimefungwa huku Halmashauri ya Mji wa Mbinga ikiwa ni mashine tatu, kwa mujibu wa Lutaja.

Taarifa za uwepo wa kikao na SANKU zilitolewa jana asubuhi na kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Mbinga Dkt Kung'e  Nyamuryekung'e wakati wa kikao cha kamati kuhusu taarifa ya utekelezaji wa shughuli za lishe Robo ya nne ya 2022/23 kilichofanyika MTC.

"Tunataka kuhamasishana na kuwapa elimu kuhusu umuhimu wa kufunga mashine hizo za kuongeza viini lishe," alisema Dkt Nyamuryekung'e ambaye pia ni mkuu wa Idara ya Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe katika halmashauri ya Mji wa Mbinga.

Alisema uamuzi huo ni utekelezaji wa moja ya maazimio ya kikao cha kamati ya lishe ngazi ya halmashauri kilichofanyika Agosti 6 mwaka huu.

Aliongeza kuwa katika kikao hicho ilibainika kuwa utoaji wa vyakula vyenye virutubisho shuleni ni changamoto kwasababu mashine za kuongeza viini lishe ni chache.Kutokana na changamoto hiyo, kamati iliadhimia kuwa wananchi wahamasishwe kulima mazao yenye viini lishe ili watoto wale vyakula vyenye lishe.




Na Alex Malanga

Afisa habari---MTC

Matangazo

  • TANGAZO KWA WAFANYABIASHARA June 04, 2025
  • TANGAZO LA KAZI August 07, 2024
  • WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA 2023 December 14, 2022
  • MATOKEO YA UPIMAJI WA KITAIFA WA KIDATO CHA PILI (FTNA) 2022 January 04, 2023
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Kheri ya Siku ya Mazingira Duniani

    June 05, 2025
  • Utoaji wa dawa za minyoo na vitamin A kuanza Juni 1 Mbinga Mji

    May 31, 2025
  • MBINGA MJI YAFANYA TATHIMINI YA LISHE

    May 29, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA DKT. SAMIA WAWASILI MBINGA MJI

    May 26, 2025
  • Tazama zote

Video

MAONYESHO YA NANENANE 2023 MBINGA
Video Zaidi

Muunganiko wa Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Mbinga District Council Website
  • Tunduru District Council Website
  • Madaba District Council Website
  • Nyasa District Website
  • Namtumbo District Website
  • Songea District Council Website
  • Songea Municipal Website

Tovuti zinazohusiana

  • NECTA
  • TAMISEMI
  • AJIRA
  • WATUMISHI PORTAL
  • NACTE
  • PREM

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Maeneo

Wasiliana nasi

    MBINGA

    Sanduku la Barua: P.O.BOX 135

    Simu ya Mezani: +225 - 2640664

    Mobile: 0733216557

    Barua pepe: td@mbingatc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faraga
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2021 MBINGA TOWN COUNCIL . All rights reserved.