English
  • English
  • Kiswahili
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara (MMM) |
    • Barua Pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Mbinga Town Council
Mbinga Town Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikao na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Mbinga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi ya Maadili
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi
      • Uchaguzi
      • Nyuki
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Afya
      • Mipango Miji na Maliasili
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo na Umwagiliaji
    • Ufugaji
    • Viwanda
    • Mawasilianao na Usafirishaji
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za maji
    • Huduma za watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
    • Ofisi ya Mbunge
  • Miradi
    • Inayotekelezwa
    • Iliyotekelezwa
    • Inayotarajia kutekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Sheria ndogo
    • Fomu mbalimbali
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Video
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
  • Shule
    • Shule za Msingi
    • Shule za Sekondari
      • Agustivo High School
      • Dr. Shein Secondary School
      • Makita Secondary School
      • Luhuwiko Secondary School
      • Mbinga Secondary School
      • Mbambi Secondary School
      • Mikiga Secondary School
      • Mbangamao Secondary School
      • Kikolo Secondary School
      • Kagugu Secondary School
      • Ndela Secondary School
      • Ngwilizi Secondary School
      • LAMATA Scondary School
      • Kindimba Secondary School
      • Lusetu Secondary School
      • Depaul Mbangamao Secondary School
      • Mkwaya Secondary School

MBINGA MJI KINARA MBIO ZA MWENGE

Tarehe ya kuwekwa: April 14th, 2024


Na Alex Nelson Malanga


Afisa Habari….Mbinga Mji


Mbinga. Halmashauri ya Mji wa Mbinga imeibuka kinara katika mashindano ya mbio za Mwenge wa Uhuru 2023 katika mkoa wa Ruvuma baada ya kuwabwaga washindani wake saba.


Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Mhe. Kanali Abbas Ahmed Abbas alisema mapema wiki hii kuwa Mbinga Mji iliibuka kidedea katika mashindano hayo baada ya kupata alama 82.98.


Waliopoteza kwa Mbinga Mji ni Manispaa ya Songea iliyopata alama 80.06, Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru (77.96), Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo (77.82) na Halmashauri ya Wilaya ya Madaba (74.93).  


Wengine ni Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga (73.57), Halmashauri ya Wilaya ya Songea (71.86) na Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa (71).


Katika ngazi ya Taifa, mkoa wa Ruvuma ulishika nafasi ya 10 baada ya kupata alama 76.27, kwa mujibu wa Mhe. Kanali Abbas aliyekuwa anazungumza wakati wa kikao cha maandalizi ya Mbio za Mwenge.


Mwaka huu mkoa wa Ruvuma unatarajia kupokea Mwenge wa Uhuru Juni 8 kutoka Mkoa wa Mtwara na kuukimbiza katika Halmashauri zake zote nane kabla ya kuukabidhi kwa Mkoa wa Njombe Juni 16.


“Tunapaswa kujiandaa kimkakati ili tufanye vizuri zaidi mwaka huu,” alisema wakati wa kikao kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Manispaa ya Songea.


Aliongeza: “Tunapaswa kufanya kila linalowezekana tuingie katika tatu bora mwaka huu.”


Ofisi ya Waziri mkuu imeandaa vigezo 10 vitakavyozingatiwa na vimeandaliwa kwa kuzingatia ujumbe wa mbio za Mwenge wa Uhuru na mahitaji ya serikali katika kipindi hiki.


Vigezo hivyo vyenye jumla ya maksi 100 ni pamoja na ufanisi wa usimamiaji wa miradi ya maendeleo (maksi 32), ufanisi katika mapokezi ya Mwenge (maksi 6), uzingatiaji wa itifaki za mwenge (maksi 8) na umahiri katika uandishi, usomaji na uwasilishaji wa risala ya utii kwa Mheshimiwa Rais (maksi 8).


Vigezo vingine ni uraghibishaji wa falsafa ya mwenge kwa mwananchi (maksi 4), uwezeshaji wa vijana (maksi 20), uwezeshaji wa makundi yenye mahitaji maalumu na ukatili wa kijinsia (maksi 4) na juhudi zinazochukuliwa katika mapambano dhidi ya VVU/Ukimwi, dawa za kulevya na Malaria (maksi 3).



Orodha ya vigezo pia inahusisha mapambano dhidi ya rushwa na changamoto za lishe duni (maksi 5) na ushiriki katika uhifadhi wa mazingira na uchaguzi wa serikali za mitaa (maksi 10).

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI June 13, 2025
  • TANGAZO NAFASI ZA KAZI May 25, 2022
  • TANGAZO KWA WAFANYABIASHARA June 04, 2025
  • WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA 2023 December 14, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • ‎JAMII YAHIMIZWA KULINDA HAKI ZA WATOTO

    June 16, 2025
  • Maadhimisho ya Mtoto wa Afrika Mbinga Mji kufanyika kata ya Kitanda

    June 13, 2025
  • Mbinga Mji Yatoa Mafunzo kwa Walengwa wa Mikopo 10%

    June 11, 2025
  • Sikukuu Njema ya EID AL ADHA

    June 07, 2025
  • Tazama zote

Video

MAONYESHO YA NANENANE 2023 MBINGA
Video Zaidi

Muunganiko wa Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Mbinga District Council Website
  • Tunduru District Council Website
  • Madaba District Council Website
  • Nyasa District Website
  • Namtumbo District Website
  • Songea District Council Website
  • Songea Municipal Website

Tovuti zinazohusiana

  • NECTA
  • TAMISEMI
  • AJIRA
  • WATUMISHI PORTAL
  • NACTE
  • PREM

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Maeneo

Wasiliana nasi

    MBINGA

    Sanduku la Barua: P.O.BOX 135

    Simu ya Mezani: +225 - 2640664

    Mobile: 0733216557

    Barua pepe: td@mbingatc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faraga
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2021 MBINGA TOWN COUNCIL . All rights reserved.