• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara (MMM) |
    • Barua Pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Mbinga Town Council
Mbinga Town Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikao na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Mbinga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi ya Maadili
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi
      • Uchaguzi
      • Nyuki
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Afya
      • Mipango Miji na Maliasili
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo na Umwagiliaji
    • Ufugaji
    • Viwanda
    • Mawasilianao na Usafirishaji
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za maji
    • Huduma za watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
    • Ofisi ya Mbunge
  • Miradi
    • Inayotekelezwa
    • Iliyotekelezwa
    • Inayotarajia kutekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Sheria ndogo
    • Fomu mbalimbali
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Video
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
  • Shule
    • Shule za Msingi
    • Shule za Sekondari
      • Agustivo High School
      • Dr. Shein Secondary School
      • Makita Secondary School
      • Luhuwiko Secondary School
      • Mbinga Secondary School
      • Mbambi Secondary School
      • Mikiga Secondary School
      • Mbangamao Secondary School
      • Kikolo Secondary School
      • Kagugu Secondary School
      • Ndela Secondary School
      • Ngwilizi Secondary School
      • LAMATA Scondary School
      • Kindimba Secondary School
      • Lusetu Secondary School
      • Depaul Mbangamao Secondary School
      • Mkwaya Secondary School

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA ORYX WAGAWA MITUNGI YA GESI 1,050

Tarehe ya kuwekwa: July 24th, 2024




Na Alex Nelson Malanga


Afisa Habari----Mji Mbinga


Mbinga. Naibu Waziri wa Nishati Mhe. Judith Kapinga kwa kushirikiana na Kampuni ya Gesi ya Oryx Tanzania jumanne (Julai 23) waligawa mitungi ya gesi 1,050 kwa wananchi wa Wilaya ya Mbinga, Mkoa wa Ruvuma.


Ugawaji wa mitungi hiyo yenye thamani ya Sh45 milioni unalenga kuunga mkono jitihada za Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan za kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia.


Kati ya mitungi ya gesi 1,050 iliyotolewa katika ukumbi wa One Pacific uliopo katika Halmashauri ya Mji wa Mbinga, Mkoani Ruvuma, kampuni ya Oryx ilitoa mitungi 700 na Mhe. Judith mitungi 350.


“Serikali kwa kushirikiana na wadau wa nishati safi ya kupikia imejidhatiti katika kuhakikisha tunaongeza matumizi ya nishati safi ya kupikia,” alisema Mhe. Judith huku akiipongeza kampuni ya Oryx kwa mchango wake wa mitungi ya gesi 700.


Kupitia Mkakati wa Taifa wa matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia (2024-2034), Serikali imedhamiria kuongeza kaya za watanzania zinazotumia nishati safi ya kupikia kutoka asilimia 10 ya sasa mpaka asilimia 80 ifikapo mwaka 2034.


Ikiwa ni sehemu ya jitihada za  kuongeza matumizi ya nishati safi, mpaka sasa Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA), imesambaza mitungi ya gesi ya ruzuku 83,500 yenye thamani ya Sh3.5 bilioni, kwa mujibu wa Naibu Waziri wa Nishati.


Kama hiyo haitoshi, aliongeza Mhe. Judith, mwaka huu wa fedha serikali imepanga kutoa mitungi 452,445 yenye thamani ya Sh10 bilioni.


“Lengo letu ni kupunguza gharama za nishati safi ya kupikia na kwa kufanya hivyo naamini tutachochea matumizi ya nishati hiyo,” alisema Mhe. Judith.


Agenda ya nishati safi ya kupikia ni muhimu sana kwa mustakabali wa maendeleo ya Taifa letu na kwa kutambua hilo Mhe. Rais Dkt. Samia amekua kinara katika kuhamasisha matumizi ya nishati hiyo.


Sifa hiyo ya Mhe. Rais haiishii Tanzania tuu, bali imevuka hadi mipaka ya nchi hii mwanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki.


Hii inadhihirishwa na yeye kuzindua ‘programu’ ya nishati safi ya kupikia Afrika yenye lengo la kuleta mageuzi na kumkomboa mwanamke.


Uzinduzi huo ulifanywa mwishoni mwa mwaka jana huko Dubai, Falme za Kiarabu wakati wa Mkutano wa 28 wa Nchi Wanachama wa Mkataba wa Mabadiliko ya Tabianchi (COP 28).


Mkurugenzi Mtendaji wa Oryx Bw. Araman Benoit alisema: “Tunataka jamii ya Tanzania iachane na nishati chafu ambayo sio mbaya kwa afya tuu, bali ni hatari kwa mazingira pia.”

Matangazo

  • TANGAZO KWA WAFANYABIASHARA June 04, 2025
  • TANGAZO LA KAZI August 07, 2024
  • WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA 2023 December 14, 2022
  • MATOKEO YA UPIMAJI WA KITAIFA WA KIDATO CHA PILI (FTNA) 2022 January 04, 2023
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Kheri ya Siku ya Mazingira Duniani

    June 05, 2025
  • Utoaji wa dawa za minyoo na vitamin A kuanza Juni 1 Mbinga Mji

    May 31, 2025
  • MBINGA MJI YAFANYA TATHIMINI YA LISHE

    May 29, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA DKT. SAMIA WAWASILI MBINGA MJI

    May 26, 2025
  • Tazama zote

Video

MAONYESHO YA NANENANE 2023 MBINGA
Video Zaidi

Muunganiko wa Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Mbinga District Council Website
  • Tunduru District Council Website
  • Madaba District Council Website
  • Nyasa District Website
  • Namtumbo District Website
  • Songea District Council Website
  • Songea Municipal Website

Tovuti zinazohusiana

  • NECTA
  • TAMISEMI
  • AJIRA
  • WATUMISHI PORTAL
  • NACTE
  • PREM

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Maeneo

Wasiliana nasi

    MBINGA

    Sanduku la Barua: P.O.BOX 135

    Simu ya Mezani: +225 - 2640664

    Mobile: 0733216557

    Barua pepe: td@mbingatc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faraga
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2021 MBINGA TOWN COUNCIL . All rights reserved.