• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara (MMM) |
    • Barua Pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Mbinga Town Council
Mbinga Town Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikao na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Mbinga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi ya Maadili
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi
      • Uchaguzi
      • Nyuki
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Afya
      • Mipango Miji na Maliasili
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo na Umwagiliaji
    • Ufugaji
    • Viwanda
    • Mawasilianao na Usafirishaji
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za maji
    • Huduma za watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
    • Ofisi ya Mbunge
  • Miradi
    • Inayotekelezwa
    • Iliyotekelezwa
    • Inayotarajia kutekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Sheria ndogo
    • Fomu mbalimbali
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Video
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
  • Shule
    • Shule za Msingi
    • Shule za Sekondari
      • Agustivo High School
      • Dr. Shein Secondary School
      • Makita Secondary School
      • Luhuwiko Secondary School
      • Mbinga Secondary School
      • Mbambi Secondary School
      • Mikiga Secondary School
      • Mbangamao Secondary School
      • Kikolo Secondary School
      • Kagugu Secondary School
      • Ndela Secondary School
      • Ngwilizi Secondary School
      • LAMATA Scondary School
      • Kindimba Secondary School
      • Lusetu Secondary School
      • Depaul Mbangamao Secondary School
      • Mkwaya Secondary School

TAKUKURU: WAANDISHI PIGENI VITA RUSHWA

Tarehe ya kuwekwa: July 30th, 2024



Na Alex Nelson Malanga


Afisa Habari----Mji Mbinga


Mbinga. Kuelekea uchaguzi wa serikali za mitaa unaotarajiwa kufanyika baadaye mwaka huu, Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) imewataka waandishi wa habari wa Wilaya ya Mbinga kuwa mstari wa mbele katika vita dhidi ya rushwa.


Akizungumza wakati wa kikao kazi na waandishi wa habari Jumatatu ya Julai 29, Mkuu wa TAKUKURU wilaya ya Mbinga Bw. Frederick Msae alisema waandishi wa habari wana jukumu la kuelimisha wananchi kuhusu haja ya kuchagua viongozi waadilifu.


“Waandishi wa habari mna uwezo wa kuwafikia wananchi kiurahisi. Tumieni vema kalamu zenu kuwaelimisha wananchi kuhusu haja ya kuchagua viongozi pasipo vitendo vyovyote vya rushwa,” alisema kamanda Msae.


Aliongeza: “Waandishi wa habari msipopiga kelele kuhusu rushwa wakati wa uchaguzi, wananchi watachagua viongozi ambao hawatakuwa na msaada wowote kwa jamii.”


Ni haja ya serikali kuona wananchi wanachagua viongozi ambao wataweza kuchanganua na kupambanua changamoto mbalimbali ambazo wanakumbana nazo katika jamii.


 “Viongozi wanaohitajika ni wale ambao watapatikana kwa njia ya haki na hivyo kuwa daraja kati ya wananchi na serikali katika mambo mbalimbali,” alisema Bw. Msae.


Bosi huyo wa TAKUKURU kwa ngazi ya wilaya alionya kuwa waandishi wa habari wasipokuwa mstari wa mbele katika kupiga vita rushwa, itaathiri imani ya hadhira yao.


Bw. Msae pia alieleza umuhimu wa waandishi wa habari kuwa wazalendo kwa nchi yao kwa kutoa taarifa za vitendo vya rushwa pindi vinapofanyika au vinapo pangwa kufanyika.


Hii, alieleza, itaisaidia TAKUKURU kuwashughulikia wahusika na hatimaye kuondoa vitendo vya rushwa katika wilaya ya Mbinga.


Pia, alisema waandishi wa habari kama kioo cha jamii, wanapaswa kuwa waadilifu kwa kutoa taarifa sahihi kwa umma pamoja na kuwanadi, pale inapobidi, wagombea wote pasipo upendeleo.


“Mnapaswa kutoa taarifa za wagombea wote bila upendeleo wowote na bila kupokea rushwa,” alihitimisha Bw. Msae.

Matangazo

  • TANGAZO KWA WAFANYABIASHARA June 04, 2025
  • TANGAZO LA KAZI August 07, 2024
  • WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA 2023 December 14, 2022
  • MATOKEO YA UPIMAJI WA KITAIFA WA KIDATO CHA PILI (FTNA) 2022 January 04, 2023
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Kheri ya Siku ya Mazingira Duniani

    June 05, 2025
  • Utoaji wa dawa za minyoo na vitamin A kuanza Juni 1 Mbinga Mji

    May 31, 2025
  • MBINGA MJI YAFANYA TATHIMINI YA LISHE

    May 29, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA DKT. SAMIA WAWASILI MBINGA MJI

    May 26, 2025
  • Tazama zote

Video

MAONYESHO YA NANENANE 2023 MBINGA
Video Zaidi

Muunganiko wa Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Mbinga District Council Website
  • Tunduru District Council Website
  • Madaba District Council Website
  • Nyasa District Website
  • Namtumbo District Website
  • Songea District Council Website
  • Songea Municipal Website

Tovuti zinazohusiana

  • NECTA
  • TAMISEMI
  • AJIRA
  • WATUMISHI PORTAL
  • NACTE
  • PREM

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Maeneo

Wasiliana nasi

    MBINGA

    Sanduku la Barua: P.O.BOX 135

    Simu ya Mezani: +225 - 2640664

    Mobile: 0733216557

    Barua pepe: td@mbingatc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faraga
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2021 MBINGA TOWN COUNCIL . All rights reserved.